AY atoa somo kwa Diamond na Kiba

Mzee wa komesho Ambwene Yesayah 'AY' awashauri Diamond na Alikiba wafanya kazi pamoja

 Ambwene Yesayah maarufu kama AY ametoa ushauri kwa Diamond na Alikiba kuweka tofauti zao pembeni na kufanya muziki pamoja.

AY ametoa ushauri huo baada ya kuulizwa na shabiki kupitia Kikaangoni cha EATV aliyetaka kujua ni msanii yupi kati ya wawili hao anayemkubali zaidi.

“Wote wawili ni wasanii wazuri na nawashauri wafanye kazi pamoja siku si nyingi,” alijibu AY.

Rapper huyo pia amewashauri mashabiki kutowachonganisha wasanii hao ambao wamekuwa na uadui wa miaka mingi.
“Upendo ndio suala la msingi,tusichonganishe watu tuweke bidii watu wafanye kazi pamoja,” aliongeza.

Hivi karibuni uhasama kati ya wasanii hao wawili wanaopendwa nchini uliongezeka zaidi hasa baada ya kumalizika kwa tuzo za KTMA ambapo walikuwa wakishindana kwenye vipengele vingi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment