Sehemu ya 3: ***KIMINI CHA MTOTO WA ASKOFU***

ILIPOISHIA Sehemu ya 2.....
Yaani sikuamini nilichokiona Duh! Nilipoifungua tu nikaka kitandani n ahata kusahau nilichokuwa ninakifanya kabla ya kuiona pochi ile. Kwa ushahidi wa vitambulisho, kadi mbili za benki, hela laki moja na ishirini na tatu, pesa tasilimu, kadi za mawasiliano za watu mashuhuri, yaani kusema ukweli niliishiwa pozi, Sitaki kuamini kama ile pochi ilikuwa ya........

ENDELEA....
Basi niliifunga pochi ile na kuiweka mezani, nami nikaendelea na Tafakari ya siku pamoja na maombi ya asubuhi!
Baadae niliswaki pamoja na kuoga na nilipokuwa tayari, nilikaa kitandani ili nifikiri kidogo kama ni sawa kuondoka nihamie pengine kwa siku inayofuata au nibaki hapo hapo tu!


Baada ya kutafakari, nilikubali kubaki hapo hapo,nikiamini lipo jambo labda naweza ng'amua na hivyo nikashuka mapokezi na kutoa taarifa kuwa bado nipo pamoja na kuacha ufunguo hapo...lakini kabla sijauliza nilijaribu kumuuliza yule kijana wa mapokezi kuwa Je kuna jina la fulani kwenye daftari lake la wageni kwa chumba kile,akasita kidogo, ila ninashukuru aliangalia na kuniambia Wengi huwa hawapendi kuandika na hata wanaoandika majina hapo,wengi huandika majina wasiyoyatumia!

Mmh kumbe! Basi nikamwaga na kumwambia nitarejea mchana ama alasiri, nikaacha funguo hapo na kuelekea zangu mishemishe!

Nilitoka nje na kujaribu kuzunguka kidogo maeneo yale na kwakweli mchana palionekana ni mahali tulivu na patakatifu mno, mbele yangu niliona kiduka hivi,nikasogea hapo jambo ninue juisi na muda wa maongezi...na wakati nakunywa juisi huku nikisubiri yule muuzaji anikwangulie vocha,nilijaribu tu kumuuliza yule ndugu.."Inaonekana maeneo haya ni hatari sana,hivi ninyi mnaishije?" Aliangalia akacheka sana na kujibu, "Najua wewe ni mgeni tu hapa,ila ukweli ni kuwa, maisha yanaenda tu na kila mmoja anafanya yake tu"

"Jana nilisikia sauti ya mtu kama akilalamika hivi na sikuona yeyote aliyekuwa hata na wazo la kutoa msaada...kwanini?" Nilimuuliza!
Basi akanijibu namna hii "Ukimkuta mtu mahali anajinyonga na watu wanapita kando huku wakimpiga picha wewe utafanyaje? Mmmh!

Niliduwaa kidogo, kisha nikalipa hela na kuanza kuondoka maana alikuwa na wateja wengi wa kuwahudumia. Nilienda nikitafakari, niliangalia huku na kule nikitembea na kujifunza kila jambo kwa kadri nilivyoweza...hakika Ukizoea kulala uvunguni,siku ukiiona dabo deka utahesabu makenchi!

Nilifika kituo cha daladala na ilipofika tu gari ilikuwa inaelekea ninakokwenda nikapanda, nilikuwa naelekea kunako maduka makubwa ili nijipatie mahitaji muhimu kunifanya nadhifu kwa yale matukio muhimu yaliokuwa mbele yangu. Nilipokuwa naingia tu kwa daladala macho yangu yaligongana na kijana mmoja ambaye alishtuka kiasi, sijui ni kwanini ila wakati ninaingia alikuwa ameweka mkono wake begani mwa binti mmoja aliyejichubua sana na kuvaa mahereni na mapambo kibao kama vile yametundikwa! Shikamoo kaka Chavala, Mmh marahaba,habari yako? Poa tu! 

Umekuja mjini kwetu kimyakimya? Nikajikuta nimemjibu...Ulitaka nipite na kipaza sauti barabarani kuwatangazia kuwa Nimekuja? Akacheka, tukacheka basi nikakaa kiti cha nyuma yake...baadae kidogo nilimsikia akimwambia yule dada, Aisee huyu kaka ni mkali Duh! Bonge la Mc na mwalimu,yaani hapa naona amenistahi maana angeweza kunipa makavu,naomba tushuke kituo kinachofuata! Nilijifanya  kama sijasikia na kimoyomoyo nikajiambia...Kama ameshatambua anakosea Inatosha! Nilimwona yule dada akiniangalia kwa woga na mimi nikatazama mbele tu...na kweli kituo kilichofuata wakashuka haraka haraka!

Basi nilikaa na kutafakari peke yangu, hivi unawezaje kukaa juu ya tawi bovu na ukawa na amani? Mawazo yangu yalikatishwa na makelele ya mama mmoja aliyekuwa anaongea na wenzake watatu waliopanda basi pale wale vijana waliposhuka
Mazungumzo yalikuwa hivi:

Yaani wanawake wengine ni wa ajabu sana,sana huwezi kuamini yule mama,mke wa mzee wa kanisa alikuwa analalamika kuwa mume wake anahisi alihujumu hela kazini kwake (huyo mama anayeongea sana alikika) Sasa hata kama ni kweli kwanini kumwaibisha mume wake hivyo? Tena mbele ya wale wamama wa kanisani....Yaani mimi kabisa siwezi kabisa kumwaibisha au kumsema vibaya mume wangu mbele za watu...Ila kweli aisee (wale wamama wengine 
wakaitikia)...akaendelea...Mimi siwezi kabisa nawambieni,kwa mfano Mimi mume wangu ni mwongo sana tu,mchafu mpaka inakera,anaweza akavaa nguo za ndani hata siku nne kama usipogomba na ninahisi amewahi kutembea na msichana wetu wa kazi...lakini kwasbabu ile ni ndoa,huwezi kunisikia mimi ninamsema vibaya kwa watu,Jamani tuzitunzeni ndoa zetu,ndio maana kiapo kilisema...Kwa shida na raha! Nakajisikia tu kucheka lakini nikajikaza,na hapo ndio hapo nikawa nashuka...Naamini yule mama pamoja na wenzake waliamini wako sawa,ila ukweli ni kuwa alikuwa anahubiri asichokiishi!

Basi huko madukani nikafanya yaliyonipeleka na kujifunza mengineyo, mchana nikaona ni wapi pameandikwa hoteli ama mahali panapouzwa chakula, nikaingia hapo kupata mlo wa alasiri, maana mchana ulikuwa umekwisha pita. Baada ya kumaliza kula nilianza safari ya kurudi hotelini, nilipofikia. Nilipofika hoteli, pale mapokezi nikakuta funguo ya chumba change haipo na nilivyoangaza huku na kule sikuwaona wahudumu na hivyo nikaamua kapanda mpaka juu na huko nikashangaa mlango wa chumba changu uko wazi na ndani nina wageni pamoja na mhudumu mmoja wapo, basi nikamuuliza mhudumu "Hawa ni wageni wangu?" akanitolea macho kwa woga na hawa wageni wakawa wanainuka kwa aibu...Samahani kaka tulijua utachelewa na hawa walitaka kupumzika tu mchana huu na kisha tungekufanyia usafi! Whaat! Nilipatwa na hasira na nikamwambia "Wewe ni mpumbavu na hawa wageni wako ni pia, mnawezaje kupumzika kwenye chumba cha mtu alichokilipia? Hamuoni nguo na vitu vingine humu? Nikiwakata kwa vitu vyangu vilivyopotea mtasemaje? ....na kwanza huu ni ushetani tu, mchana huu wametoka wapi mpaka wapumzike na tena wapumzike mchana tu? Samahani sana kaka, tusamehe yaishe!

Nikawageukia wale wapumzikaji wakiwa mlangoni na kuwaambia "Mnapoikaribia dhambi ni tamu sana lakini saa madhara yake yatakapowatafuna ndio mtakumbuka kuwa chumvi sio kiungo tu bali ni dawa pia!

Wakatoka na kuendelea na mizozano yao hapo nje, mimi nikafunga mlango na kuendelea na mambo yangu. Nikapumzika kidogo mimi kwa niaba yao, maana niko chumbani kwangu, kisha nikaenda kuoga na kujiandaa kwa ajili ya ile harusi niliyokuwa nasherehesha Usiku ule!

Nilitoka nimeulamba kiasi cha kila mmoja kunikata jicho...najua vichwani mwao walikuwa wanafikiri mimi mwenzao sema tu hawajui mimi nani. Nikatoka mpaka nje kabisa na nikachukua bajaji na kwenda ukumbini, nilifika kwa wakati na kwenye ladi za mwaliko walisema tutaanza saa kumi na mbili, basi kwasababu zao wenyewe wakachelewa kuja na hivyo muda huo nikawa natafakari siku nzima ilivyokwenda tangu nimeingia mjini hapa.

Majira ya saa moja na nusu maharusi walifika na ikabidi niende kuwaona na kuongea nao jinsi inavyopaswa kuwa na kusikia mapendekezo yao kama yapo ili kuifanya siku yao njema sana. Nilipofika pale nikakuta bibi harusi anatapika,nikashtuka sana nikidhani anaumwa...lakini yule msimamizi wa kiume akajikuta ameropoka "Hata mke wangu yule mtoto wetu wa kwanza,miezi ile ya mwanzo mwanzo alitapikaga sana yaani" Basi hapo nikawa na majibu na nikachefuka sana maana sipendagi sana kuwa shahidi wa mambo haya, Ndio! Sijakosea, nimesema sipendelei sana kusherehesha harusi zilitoka fungateni tayari,maana mimi ni mtumishi na hata Ushereheshaji kwangu ni madhabahu!

Nikawauliza hivi mmefungia ndoa yenu wapi vile? Akataja jina la kanisa fulani la pentekosti....Nikawauliza mchungaji anakuja hapa ukumbini? na Je anajua ukweli huu? Wakajibu kwa pamoja kwa kingereza No! No! No! Mfalme Chavala ni ajali hizi za ujanani tu, hajui na isingekuwa rahisi hivi kama tungesema, Tunajua tumekosea na tutatengeneza tu, utusamehe na wewe pia na tunaomba utusitiri!

Nikawaambia mimi naweza kusema ndio lakini mnajua mmedanganya madhabahuni na mkala kiapo katika uongo? Nikawambia maandiko katika Mithali 28:13 yanasema "Afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali aziungamaye atapata rehema" Nikapiga Injili kidogo hapo na kwakuwa nilikuwa siwahukumu wala kuwachukia, ila nilikuwa nasema nao kwa faida ya maisha yao huko mbeleni, ninashukuru walinielewa na nikwaacha watafakari kwa kina na kuona wanaona wafanye nini; Nikawasisitiza... msipotengeneza hii kitu itawatafuna, ila ni bora dini iwatenge kwa muda kuliko kwenda mafichoni na baadae mkajifungia mafanikio, wakaniambia poa Chavala, tutaangalia hilo jambo, haya basi nikawaauliza yale mengine kuhusu sherehe na tulipomalizana nikawambia wajiandae na mimi nikaanza kazi yangu, tena nikiwa na amani moyoni kuwa niwaambia ukweli na lipi wanapaswa kulifanya!

Kama kawaida, nikawakaribisha wazazi wa pande zote mbili,wakafuata wapambe na kisha maharusi na nikawaacha wakacheza sana nyimbo walizochagua. Baada ya Ukaribisho wa mwenyekiti wa kamati, nikaambiwa nimwite Mtume fulani aje kufungua sherehe rasmi kwa maombi!
Basi nikamwita kwa jina na mara akatokea ndugu mmoja ndani ya suti kali na akiwa anakuja nikawa namwangalia vizuri...mbona kama mtu huyu ninamjua ila simjui vizuri,nikampa kisemeo naye akaniangalia sana usoni na kisha akasema neno kidogo na kuomba!
Aliporudi kukaa bado nilikuwa napambana kukumbuka nimemwona wapi na nikajikuta kwenye kisemeo nimesema…..Ahsante sana mtumishi wa Bwana, nafikiri tumeonana mahali ila nitakuja nikusalimie tu mezani kwako Haleluya!

Basi baada ya Utambulisho,keki na Shampeni,wageni waalikwa wakiwa wanacheza nikawa napumzika kidogo,Nikashangaa tu mtu amenigusa begani na kunivuta mpaka nyumba ya Ukumbi,Kumbe alikuwa ni yule mtumishi na hapo nikawa nahisi kama Je ni yule niliyemwona pale nilipofikia jana au lah!

Akaniambia "Chavala! Kazi ni nzuri sana, Hongera! Nakufuatilia sana, ila samahani, kuna wakati huwa majaribu yanatusonga kwa upesi ila Nakuahidi nitajirekebisha! Mmh! Jamani mbona sijakuelewa kwani kimetokea nini? Nikamuuliza, Akasema Chavala watu huwa wanakosea,hata mimi huwa nakosea, nikamtolea macho!

Akawa kama anashindwa kuongea na kushindwa kujiamini...Lakini kwa kujikaza akasema Chavala mimi ni.......ITAENDELEA!

(c)King Chavvah, 2015
+255 713 883 797
Instagram: kingchavvah
Twitter @kingchavala
E-mail; lacs.project@gmail.com
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment