Oscar Pistorius Kuachiwa Ijumaa Ya Wiki Hii

 Oscar Pistorius akiwa na mpenzi wake Reeva Steenkamp.
 Oscar Pistorius akiwa mahakamani wakati wa kesi yake.



Mwanariadha Oscar Pistorius.
AP_oscar_pistorius_reeva_steenkamp_jt_140302_16x9_992
Mwanariadha mahiri wa nchini Afrika Kusini, Oscar Pistorius anatarajiwa kuachiwa Ijumaa hii baada ya kuonyesha tabia nzuri akiwa gerezani. Pistorius alihukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani mwaka uliopita kwa kosa la kumuua mpenzi wake, Reeva Steenkamp katika usiku wa Siku ya Wapendanao 'Valentine's Day'. 


Pistorius ametumikia kifungo cha miezi 10 pekee gerezani kati ya miaka mitano aliyohukumiwa. Baada ya kuachiwa, Pistorius anatarajiwa kuwa akitumikia muda wake uliobaki akiwa katika kifungo cha nje.
Wakati akitoa hukumu ya staa huyo, Jaji Thokozile Masipa alisema kuwa kiongozi wa mashtaka nchini Afrika Kusini alishindwa kuthibitisha kuwa Pistorius alikusudia kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp alipompiga risasi nyumbani kwake akidhani kuwa ni mwizi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment