Mzee Yusuf Apanga Kuutafuta Ubunge

Msanii wa muziki wa Taarab nchini na mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarabu, Mzee Yusuf amesema ana mpango wa kuacha muziki na kuingia kwenye siasa.

Akizungumza kwenye kipindi cha Tam Tam za Mwambao cha East Africa Radio, Mzee Yusufu alisema anatarajia kutoa album mbili za mwisho ili aweze kuachana na muziki na kujikita zaidi kwenye siasa na usimamizi wa bendi yake.

“Muda ukifika nitaacha, lazima niache muziki kwa sababu nina mambo mengi ya kufanya nje ya muziki,” alisema.

“Na kama hivyo nikipita katika nafasi ya ubunge itabidi tu nichague moja, itabidi kwenye muziki nisipatikane kwa asilimia mia moja hivyo wapenzi wa muziki wangu lazima waelewe kuwa naacha muziki kwa sababu ya siasa na kazi zangu zingine ambazo ni nyingi na zinahitaji uwepo wangu, hivyo lazima niache muziki ili niweze kukamilisha mambo mengine nikiwa nje ya muziki.”

Crdt: EATV
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment