Msajili Avipiga Mkwara CCM, Chadema, CUF

Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi amevitaka vyama kurekebisha katiba zao kwenye kipengele kinachoruhusu kuanzishwa kwa vikosi vya ulinzi na usalama.
Vyama vyenye vikosi cha ulinzi na usalama ni Chadema chenye Red Brigade, CCM (Green Guard), CUF (Blue Guard) na sasa ACT-Wazalendo (ACT Amani).
Mutungi alisema uanzishwaji wa vikundi hivyo unakwenda kinyume na Katiba ya nchi inayolipa jeshi la polisi mamlaka ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Akizungumza baada ya mkutano wake na vyama hivyo jana, Jaji Mutungi alisema katiba za vyama vingi vilivyosajiliwa kabla hajaingia ofisini vilikuwa na kifungu kinachoruhusu kuanzishwa kwa vikosi vya ulinzi na usalama wa mali za chama au viongozi wao wawapo katika mikutano.
“Haturuhusu kifungu hicho kuwapo kwenye katiba za vyama vinavyosajiliwa sasa (hakugusia ACT - Wazalendo). Hatuvifundishi vyama vya siasa namna ya kuandaa katiba zao lakini tunasimamia kifungu hiki kwa vile kinapingana na sheria.”
Jaji Mutungi alisisitiza kuwa vyama vya siasa nchini havina uelewa wa sheria ya vyama vya siasa ambayo ndiyo inayovisimamia, ndiyo maana vinashindwa kuendesha shughuli zao kwa mujibu wa sheria hiyo.
Kauli ya polisi
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Ernest Mangu alisema watapambana na vikundi vya ulinzi na usalama ndani ya vyama vya siasa wakati wa Uchaguzi Mkuu endapo vitaingilia majukumu ya jeshi la polisi.
Alisema uanzishwaji wa vikundi hivyo ni kinyume cha sheria inayolipa Jeshi la Polisi dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Alisema vikundi hivi vilianzishwa kama chipukizi au halaiki lakini baadaye vilikuwa na kubadili malengo na kuanza kuingilia majukumu ya polisi na kuhatarisha amani.
Maoni ya wadau


Hata hivyo, kauli za Msajili na Mangu zilipokewa kwa hisia tofauti na viongozi wa vyama hivyo na baadhi vikiweka wazi kuwa havipo tayari kuachana na vikundi hivyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment