Mtanzania Anayedaiwa Kuhusika na Ugaidi Kenya Kuhukumiwa Leo

Mtanzania aliyekamatwa Kenya akidaiwa kuhusika na tukio la ugaidi katika Chuo Kikuu cha Garissa lililosababisha vifo vya watu 150, Rashid Charles Mberesero (20) alikuwa ni mwanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya sekondari ya Bihawana, lakini uongozi wa shule alipokuwa anasoma umesema alitoweka shuleni hapo tangu mwezi Desemba mwaka jana.
Habari zilizothibitishwa na wazazi wake ni kuwa mwanafunzi huyo anasoma katika Shule ya Sekondari ya Bihawana Dodoma mara baada ya kufaulu katika Shule ya Sekondari Gonja mkoani Kilimanjaro.
Taarifa hizo zimekuja wakati Mberesero maarufu kwa jina la Rehani Dida, akitarajiwa kufikishwa mahakamani leo jijini Nairobi baada ya watuhumiwa wengine kufikishwa mahakamani juzi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment