Chama Cha Kutetea Abiria (CHAKUA) Yaitaka SUMATRA Kushusha Nauli kwa Daladala na Mabasi ya Dar es Salaam

Mwenyekiti
wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa(Chakua),Hassan Mhanjama akionyesha
barua kwa waandishi wa habari  (hawapo pichani) ambazo wamejibiwa na
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) katika
Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Jijini Dar es Salaam.
Chama Cha Kutetea Abiria (Chakua) kimesema kuwa kutokana na bei ya mafuta kushuka nchini nauli ya daladala na nauli ya mabasi mikoani inatakiwa kushuka kwa asilimia 25.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Mwenyekiti wa chama hicho,Hassan Mhanjama amesema Mamlaka ya Usafiri wa Maji na Nchi Kavu (Sumatra) ina wajibu wa kuitisha mkutano na wadau kujadili kushuka kwa gharama ya nauli ili mwananchi aweze kunufaika bei ya kushuka kwa mafuta.
Mhanjama amesema kwa nauli ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa Kilomita 10 ya sh.400 inatakikwa kushuka na kufikia sh.300 na nauli ya mkoani ya Sh.40,000 inatakiwa kushuka na kufikia sh.30,000.
Amesema kuwa wamiliki wa Daladala na mabasi ya mikoani kusema bei ya vipuli na tairi zimepanda haihusiani na kushuka kwa bei ya mafuta kwani wakati mafuta yanapanda wanalamika na bei kupandisha hivyo sasa wanalazimika kushusha nauli zao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment