Chanjo Mpya ya HIV Yatoa Mafanikio

Kwa mujibu wa ripoti ya Wanasayansi nchini Marekani, mbinu mpya ya chanjo imeonekana kuwakinga nyani dhidi ya virusi vya HIV.
Kwa kawaida chanjo huifundisha kinga ya mwili wa mtu kukabiliana na maambukizi.
Lakini,watafiti katika taasisi ya Scripps mjini Carlifornia wamebadilisha DNA ya nyani hao ili kuzipa seli zao uwezo wa kukabiliana na virusi vya HIV.
Kikosi hicho cha wanasayansi kimetaja hatua hiyo kama mafanikio makubwa na sasa kinataka kuanzisha mbinu hiyo miongoni mwa binaadamu.
Majaribio yaliofanywa miongoni mwa nyani hao katika ripoti ya jarida la asili,yalionyesha kuwa nyani walikingwa kutokana aina yoyote ya virusi vya HIV kwa kipindi cha wiki 34.
Watafiti wanaamini kuwa mpango huo huenda ukawa muhimu miongoni mwa watu ambao wana virusi vya HIV.
Mtafiti bingwa Professa Micheal Farza amesema, ‘tunakaribia kupata tiba ,lakini bado tunakabiliwa na vikwazo hususani katika usalama wa kuwapa watu wengi zaidi.
Chanjo za HIV zimeshindwa kufanikiwa kwa kuwa virusi hivyo hujibadilisha mara kwa mara kila vinapolengwa na dawa, lakini Chanjo hii mpya hulenga eneo ambalo virusi hivyo hujibadilisha.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment