Mwanasheria Mkuu: Ripoti ya Mabilioni ya Uswisi Ipo Tayari

Kamati iliyoundwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kuchunguza mabilioni ya fedha yaliyofichwa na baadhi ya Watanzania katika benki mbalimbali nchini Uswisi, imekamilisha uchunguzi na inasubiri kukabidhi ripoti ya kazi hiyo kwa Spika wa Bunge.
Hayo yalisemwa jana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alipokuwa akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, Dar es Salaam.
Masaju alisema kamati hiyo ilikamilisha kazi yake baada ya kuwahoji watu mbalimbali na kukamilisha kazi hiyo kama walivyoagizwa na Bunge na kinachosubiriwa ni kuikabidhi kwa chombo hicho cha kutunga sheria.
“Ofisi yangu kupitia kamati iliyoundwa tulikwishamaliza kazi hii, lakini hatuwezi kutoa taarifa kupitia sehemu nyingine zaidi ya ofisi iliyotupatia kazi kama utaratibu unavyoelekeza.
“Sasa wananchi na nyie waandishi wa habari msubiri taarifa hiyo itolewe kule bungeni ambako tuhuma hizi zilianzia,” alisema Masaju.
Watuhumiwa
Vigogo 10 wametajwa kuhusika katika kashfa hiyo. Inadaiwa kuwa katika orodha hiyo, yupo kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu, maofisa watatu wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), mawaziri wastaafu ambao baadhi yao bado ni wabunge na aliyewahi kuwa kiongozi mwandamizi wa Benki Kuu Tanzania (BoT).
Kamati ilivyoundwa
Kamati hiyo maalumu iliundwa kwa Azimio la Bunge baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kuibua tena tuhuma hizo bungeni mapema mwaka jana, akidai kuna vigogo walioficha Sh323.4 bilioni katika benki mbalimbali za Uswisi.
Kiasi hicho cha fedha kinaweza kujenga barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 300 ambao ni sawa na kutoka Morogoro hadi Iringa.
Kwa mara ya kwanza, tuhuma hizo zilitolewa bungeni na Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), mwaka 2012.
Katika kikao cha Tisa cha Bunge, Zitto aliwasilisha hoja binafsi kulitaka Bunge kuchunguza na kuielekeza Serikali kuchukua hatua dhidi ya Watanzania aliowaita vigogo walioficha fedha na mali haramu nje ya nchi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment