Serikali Yakana Kuwaua Waandamanaji DRC

Serikali inasema kwamba walinzi wa maduka binafsi ndio waliowaua waandamanaji
Serikali ya jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imekanusha madai ya kuwauwa waandamanaji waliokuwa wakiandamana kupinga mapendekezo ya kubadilisha sheria za uchaguzi mkuu.
Makundi ya kutetea haki za binadamu, yanasema kuwa zaidi ya watu arubaini wameuawa katika siku tatu za ghasia.
Waziri wa mawasiliano Lambert Mende, aliambia BBC kwamba polisi hawakutumia silaha zozote dhidi ya waandamanaji hao.
Alisema waandamanaji ambao aoliwataja kama waporaji, waliuawa na walinzi waliokuwa wanalinda majengo ya biashara yaliyoporwa
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema kwamba zaidi ya watu 40 wameuawa katika siku tatu za vurugu mjini Kinshasa.
Mabadiliko yaliyopendekezwa huenda yakachelewesha uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao, wakati Kabila anatarajiwa kung'atuka baada ya kuitawala nchini huo kwa miaka 14.
Credit: BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment