Waziri Simbachawene: Nitafuatilia Usiri wa Mikataba, Lakini Sasa Nasoma Mazingira

Waziri wa Nishati na Madini ,George Simbachawene amesema kuwa watanzania wamuamini ataendeleza kwa kasi ile ile katika kuwafikishia wananchi maendeleo kupitia sekta za nishati na madini.

Hayo ameyasema leo wakati alipoanza kazi rasmi katika Wizara hiyo akichukua nafasi ya Profesa Sospeter Muhogo aliyejiuzulu wiki iliyopita,amesema kila mtu sio mkamilifu hata mitume watu wengine hawakumuamini.

Simbachawene amesema ana uzoefu wa kufanya kazi na kuachana na vyeti kwani vyeti ni ziada lakini kalama ya uongozi ndiyo inayohitajika.

Aidha amesema wanaotilia shaka uteuzi wake watakuwa na kigezo lakini kila mtu hawezi kuamini kila binadamu ana mapungufu kwa namna anavyoona mtu.

Simbachawene amesema atafuatilia usiri wa mikataba lakini sasa anasoma mazingira kwanza na kuweza kuweka bayana suala hilo.

“Niko hapa watu waniamini kutokana na kazi zangu na watanzania waniamini niweze kufanya kazi niliyoaminiwa kwa niaba ya watanzania wenzangu”amesema Simbachawene.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment