Wolper Asikitika Jina Lake Kutumiwa na Coca Cola Bila Hata Kushirikishwa Wala Kulipwa!!!

Msanii wa Bongo Movie Nchini Jackline Wolper amewatupia lawama kampuni ya Vinywaji vya Coca Cola nchini kwa kutumia Jina lake bila ya makubaliano maalumu ya Kibiashara.

Alisema hayo kupitia ukurasa wake wa Istragram muda mchache kutoka sasa ni hichi ndicho alichoweza kuandika...

“Habari Followers pamoja na wa Tanzania wote ambao naamini huwa mnaingia katika page yangu ya insta.Nimepokea zawadi hii ya Coca cola kwa siku 6 .

Na sio kwamba sikutaka kupiga picha kama wenzangu au ku post kama wenzangu,  nilikuwa natafakari kweli kampuni kubwa ya kitaifa na kimataifa inaweza kutumia gharama kubwa kuandika majina yetu bila kuchukuwa hata nafasi na heshima kubwa tuliyonayo kutushirikisha tu katika makubaliano ya kuandika majina yetu katika makopo yao.

Maana naamini mafan's wa Wolper wangeweza kushare na Coca cola kutokana Jina Langu kuwa label katika makopo yao.

Sasa Naamini tuna wanaharakati,wabunge,wanaSheria pamoja na serikali ambao huwa wanafwatilia wale wauza CD wa kariakoo basi Naomba Juhudi hizi mzihamishie huku katika kampuni hii kubwa ya kimataifa Coca cola ili kutetea haki za wasanii na sio kudhalilishwa kwa kiasi hiki jamani.

Sijui kama wasanii wenzangu walilipwa siwezi kuwasemea lakini haya ni mawazo yangu binafsi”. Wolper aliishia hapo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment