Crouch Akataa Kurejea London Kujiunga na Bosi Wake

Mshambuliaji kutoka nchini England, Peter James Crouch amezima ndoto za aliyekua meneja wake Tony Pulis za kutaka kumuhamisha huko Stoke On Trent na kumpeleka jijini London kwa ajili ya kujiunga na klabu ya Crystal Palace.
Crouch, amezima ndoto hizo baada ya kukubali kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu ya Stoke City ambao utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka 2017.
Pulis, alitarajia kumsajili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 33 kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu, kufuatia mkataba wake wa awali kutarajia kufikia kikomo mwishoni mwa msimu huu.
Hata hivyo Crouch aliungana na mchezaji mwingine wa Stoke City, Glenn Whelan ambaye amakubali kuongeza mkataba mpya kwa muda wa miaka miwili ijayo.
Tonny Pulis wakati akiwa mnejea wa Stoke City alimsajili Crouch mwaka 2011 akitokea kwenye klabu ya Tottenham Hostpurs ya jijini London.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment