Waziri Awaomba Radhi Wanafunzi Kenya

Waziri wa usalama nchini Kenya Joseph Nkaissery amewaomba radhi wanafunzi wa shule ya msingi waliofyatuliwa gesi ya kutoa machozi wakati walipokuwa wakiandamana kupinga unyakuzi wa kipande cha ardhi ambacho kilikuwa uwanja wao wa kuchezea.
Bwana Nkaissery amempa mnyakuzi wa ardhi hio siku moja kuondoa sehemu ya ukuta iliobaki baada ya wanafunzi kuuangusha na kisha kuondoka katika eneo hilo.
Wanafunzi waliofyatuliwa mabomu ya kutoa machozi kwa kuandamana kupinga unyakuzi wa uwanja wao
Nkaisery ameongeza kwamba serikali itaweka uzio katika ardhi hio na kuiwacha kuwa uwanja wa kuchezea wa wanafunzi hao.
Wakati huohuo, amewaonya wanaharakati dhidi ya kukiuka sheria kila wakati wanapojiandaa kufanya maandamano badala ya kuchukua sheria mikononi mwao. 
Mnamo Jumatatu, wanafunzi watano na polisi mmoja walijeruhiwa katika vurugzu zilizotokea baada ya wanafunzi kuandamana kupinga unyakuzi wa ardhi yao kutoka kwa mtu aliyekuwa na mipango ya kufanya ujenzi.
Wakenya wamekosoa polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya wanafunzi , hali ambayo imesababisha afisa ammoja mkuu kusimamishwa kazi kwa mda.
Shirika la kutetea masilahi ya watoto, la Save The Children, pia limelaani kitendo cha polisi dhidi ya wanafunzi hao ambao walikuwa wanaandamana kwa amani kutetea uwanja wao uliokuwa umenyakuliwa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment