Kikwete: Mwanamke Anaweza Kuingia Ikulu Mwaka 2015

Uchaguzi mkuu wa Urais pamoja na wabunge unatarajiwa kufanyika mwezi oktoba mwaka huu ambapo joto la kisiasa limeanza kupanda huku vyama vya siasa vikihaha kuhakikisha kwamba wanaingia Ikulu Magogoni jijini Dar es salaam.
Mwaka huu wanawake wamezidi kuhamasika na kuhamasishwa   kutangaza nia ya kuingia katika kinyang’anyiro cha kugombea urais nchini Tanzania suala ambalo linaweza kubadilisha historia ya Tanzania  kwa kuwa  miaka marais  wote waliowahi kuongoza nchini Tanzania  hakuna Rais Mwanamke.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kitaifa yalifanyika  mkoani Morogoro,  Rais Kikwete amezidi kuwatia  hamasa Wanawake kufuatia kuwataka  kujiamini na kutohofia kuwania urais huku akisisitiza kuwa wanawake wanaweza na hawakuwahi kumuangusha.
Ameongeza kwa  kuwataka  wanawake waache uoga wa vitisho vya aina yeyote kwa kuwa  wengi wao wameonesha uwezo mkubwa katika nafasi mbalimbali za uongozi katika kipindi cha awamu yake.
Ushirikishwaji wa wanawake katika uongozi umeifanya Tanzania kuwa mingoni mwa nchi 20 zinazo ongoza dunia na nchi ya tano katika bara la Afrika katika suala la uwezeshaji wa wanawake.Suala linalothibitisha kwamba wanawake wanaweza kuliongoza taifa la Tanzania.
Hadi sasa kuna nchi sita duniani zinazoongozwa na wanawake. Nchi hizo ni Korea Kusini Bi Park Geum-hye, Ellen Johnson Sirleaf  rais wa Liberia, Dilma Vana Rousseff ni rais wa Brazil, Cristina Fernández de Kirchner rais wa Argentina, Tarja Kaarina Halonen ni rais wa nchi ya Finland, pamoja na Sheik Hasina Wajed rais wa sasa wa Bangladesh.
Katika hatua nyingine Takwimu zinaonesha kuwa  wanawake Mawaziri wapo 16, manaibu 20, Makatibu wakuu 8, Naibu katibu wakuu 19 Majaji 40, Mabalozi 13, Wakuu wa mikoa 11, Makatibu Tawala 13 na wakuu wa wilaya 71.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment