Breaking News: Kocha wa Timu ya Taifa Stars Sylvester Marsh Afariki Dunia

Kocha Sylvester Marsh amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Marsh alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya koo na hivi karibuni alisafirishwa kutoka Mwanza hadi jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, hali ya Marsh aliyewahi kuwa Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Kilimanjaro Stars pia alizinoa timu kadhaa za Ligi Kuu Bara iliendelea kuwa mbaya kadiri siku zinavyosonga mbele.

Pamoja na hivyo suala la afya yake liliendelea kuwa siri kubwa huku baadhi ya wadau wakisumbuka kutafuta wodi aliyolazwa.

Aliwahi kuugua taabani na kukawa na taarifa za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumtelekeza. Lakini baadaye lilikanusha.

Mdau, Abdulfatah Saleh ambaye ni mmiliki wa Hoteli ya Sapphire Court ya Kariakoo jijini Dar es Salaam ndiye alijitolea kumhudumia katika matibabu yake.

Ingawa alikuwa hapendi watu wajue, lakini mdau huyo ndiye alifanya kila, juhudi kuhakikisha Marsh anapata matibabu bora hadi alipopata nafuu na kurejea kwao Mwanza.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment