Maalim Atembelea Ofisi za CUF Zilizoteketezwa kwa Moto

Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF ambaye pia ni Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ametembelea ofisi ya Chama hicho iliyoteketezwa kwa moto na watu wasiojulikana kwenye jimbo la Dimani.
Mara baada ya ukaguzi huo Maalim Seif  alisema kitendo hicho ni cha kulaaniwa na hakipaswi kufanyika katika kipindi kama hiki.
Alisema matendo ya namna hii yalikua yakifanyika katika zama za siasa za Chuki visiwani Zanzibar ambapo kwa sasa zimeondoshwa baada ya uwepo wa serikali ya umoja wa kitaifa.
Aidha Maalim Seif ametoa wito kwa wanachama wa Chama cha CUF kutolipiza kisasi kwani kufanya hivyo kutasababisha uwepo wa uvunjanji wa Amani.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment