Gazeti la Kenya Laomba Radhi Kuchapisha jalada “Charlie Hebdo” Linamuoneesha Mtume Mohamed {S.AW}

Gazeti la Charlie Hebdo likiwa na katuni ya Mtume Muhammad.

Gazeti la Kenya limeomba msamaha kwa kuchapisha jalada la gazeti la Charlie Hebdo, kwa kumchora Mtume Muhammad kufuatia kilio kutoka kwa wasomaji Waislamu.

Mchora katuni wa gazeti la Charlie Hebdo Renald Luzier a.k.a Luz (katikati) akifarijiwa na wenzake wakati wa mkutano na waandishi wa habari akizungumzia sakata lililotokana na kumchora Mtume Muhammad kwenye gazeti hilo.

Gazeti la Star “limejutia sana” kwa kosa lolote lililosababishwa na “uchapishaji mpya mdogo” wa jalada.

Mchora katuni wa gazeti la Charlie Hebdo Renald Luzier a.k.a Luz akionekana kuguswa na suala hilo wakati wa mkutano na waandishi wa habari.
Wakati huo huo, gazeti la pili la Kenya limechapisha jalada lenye lugha ya matusi ya kuchekesha likiwa na makala inayosema inashikilia uhuru wa vyombo vya habari.
Nchini Senegal, serikali imekataza usambazaji wa jarida hilo la Ufaransa.

Wasenegali wengi ambao ni Waislamu wanaonekana kukubali katazo hilo, anasema mwandishi wa habari.
Nchini Ufaransa baadhi wa wasomaji waliamua kurudisha nakala za gazeti hilo.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment